Pizza Ya Viazi
Vipimo
Unga wa ngano - 3 Vikombe vya chai
Chumvi - 1 1/2 Kijiko cha chai
Sukari - 3/4 Kijiko cha chai
Maji - 1 3/4 Vikombe vya chai
Hamira - 1 Kijiko cha chai kilichojaa
Viazi - 2 Vikubwa
Kitungu - 1 kidogo
Mafuta ya Zeituni - 4 Vijiko vya supu
Namna ya kutengeneza na kupika
Changanya unga, 1/2 kijiko cha chai chumvi, sukari, na hamira katika mashine,na mimina maji pole pole.Uwache unga ukandike vizuri hadi ilainike.
Ufunike na uache uumuke kwa masaa 2 au zaidi.
Tayarisha viazi kwa kuzikata slesi na kuziroweka ndani ya maji ya baridi ili isigeuke rangi.
Kisha mwaga maji na uweke chumvi 1/2 kijiko cha chai, iwache kwa dakika 5 hivi ili itowe maji na uyamwage.
Kisha changanya viazi, kitungu kilichokatwa, na mafuta ya zeituni kijiko 1, nauweke kando.
Washa oveni moto wa 440F.Tayarisha trei ya kuchomea kwa kuipaka mafuta.Kisha tandaza unga (uliokwisha fura), ukitumia mikono yako na kusambaza hadi pembeni mwa trei.
Panga viazi, nyunyiza chumvi 1/2 kijiko cha chai, pilipili manga ya unga na mafuta ya zeituni vijiko 3 iliyobakia.
Pika hadi pizza iwachane pembeni na kuwa rangi ya dhahabu, kama dakika 30 hivi.
Epua, na iwache ipowe kidogo;kata vipande na itakuwa tayari kuliwa.
Thursday, May 17, 2018
PIZZA YA VIAZI(POTATOES PIZZA)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Fish balls
FISH BALLS MAHITAJI Tuna vibati viwili (au samaki asiekuwa na miba wa kiasi) Cheese 3/4 cup (tea cup) iloparwa Carrot ndogo 1 (iloparwa ...
-
MKATE WA MCHELE/MKATE WA KUMIMINA Mahitaji 1.Unga wa mchele (rice flour 2 vikombe vya chai) 2.Sukari (sugar 3/4 ya kikombe cha chai) 3...
-
Naomba nikujuze mambo matano muhimu yakuimarisha afya yako ila kumbuka awali ya yote mazoezi ni muhimu kwa afya yako. 1. unaishi sehemu yen...
-
FISH BALLS MAHITAJI Tuna vibati viwili (au samaki asiekuwa na miba wa kiasi) Cheese 3/4 cup (tea cup) iloparwa Carrot ndogo 1 (iloparwa ...
No comments:
Post a Comment