.Visheti vya kokoto
MAHITAJI
siagi robo
Sukari robo
Maziwa ya unga vijiko 2 vya chakula
Baking powder kjk 1cha chakula
Unga wa ngano nusu
Yai 1
Vanilla au ladha yoyote kijiko 1
Mafuta ya kupikia nusu lita
MATAYARISHO
Saga sukari na siagi pamoja mpaka ilainike weka yai.
mix vizuri halafu weka unga, vanila kijiko kimoja, baking powder na unga wa maziwa changanya vizuri.
weka maji kidogo kidogo kwenye mchanganyiko wako mpaka uwe donge moja USIJAZE maji na wala usiwe mgumu sana.
Ugawe madonge 8
chukua kila donge sokota kama kamba na ukate vipande vidogo vidogo dizain ya kokoto,,
weka mafuta jikoni yakipata moto weka visheti vyako mpaka viive visiwe vyekundu sana.
toa viweke pembeni vipoe.
MATAYARISHO ya shira
👇👇
Weka sufuria kwenye jiko weka maji kikombe kimoja na sukari kikombe kimoja, acha ichemke mpaka iwe nzito
utaona inaaza kuganda pembeni mwa sufuria
weka vanilla na visheti punguza moto uwe mdogo
Mix mpaka viwe vikavu kabisa (vizuri kuvi mix kwa kuliinuwa sufuria na kuvipeta ili visivurugike). Tayari kwa kuliwa
Thursday, February 20, 2020
Vish
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Fish balls
FISH BALLS MAHITAJI Tuna vibati viwili (au samaki asiekuwa na miba wa kiasi) Cheese 3/4 cup (tea cup) iloparwa Carrot ndogo 1 (iloparwa ...
-
MKATE WA MCHELE/MKATE WA KUMIMINA Mahitaji 1.Unga wa mchele (rice flour 2 vikombe vya chai) 2.Sukari (sugar 3/4 ya kikombe cha chai) 3...
-
Naomba nikujuze mambo matano muhimu yakuimarisha afya yako ila kumbuka awali ya yote mazoezi ni muhimu kwa afya yako. 1. unaishi sehemu yen...
-
Huu ni mchanganyiko ambao unakupa nguvu na afya,kuna vitu vitano ambavyo vyote ni muhimu kwa afya yako humo 1,,ndizi 2;;parachichi 3;;app...
No comments:
Post a Comment